GENERATION OF LOVE UNIT

GENERATION OF LOVE UNIT
GENERATION OF LOVE@2013

Wednesday, August 28, 2013

SAM WA UKWELI vs COUNTRY BOY ndani ya ROYAl BASH WAITIKISA DAR ES SALAM,,WAKALI KIBAO KUSHAMBULIA JUKWAA WEEKEND HII, Bonya hapa kujua zaidi




                                                              
Ule mpango wa kuendeleza kula bata na wala bata ndani ya Jiji la Dar es salaam utafikia kikomo jumamosi hii ndani ya ukumbi wa Mombasa uliopo Sinza oppositte na Hotel ya lion, ambako wale watoto wazuri wa Vyuo vyote Dar es salaam watakutana na ma Braza kaka wa ukweli kuruka kwanja za ukweli kutoka kwa ma Dj wakali Tanzania na kushuhudia nan mkali stajini kati ya Country Boy , Kacci , Sam wa ukweli  pamoja na Vijana wakali wa michano hivi sasa na wazungumzia The Run entertainment. wakisindikizwa na Vipaji lukuki kutoka katika vyuo tofauti Tanzania kwa kiingilio cha bei ndogo tu ya sh.5000, kwanzia kumi jioni hadi jogoo awike asipo wika mzigo utaendelea huku watu kumi wa kwanza kuingia ukumbini watapata bia  mbili kwakila mmoja kutoka kwa Jonstwice......Mzigo huu mzima umesimamiwa na ROYAL COLLEGE OF TANZANIA

Wednesday, August 14, 2013

Mwanafunzi wa Marangu Sec atekwa na kufanyishwa ngono hotelini siku 4 mfululizo....Bonya hapa kujua zaidi


MWANAFUNZI wa kidato cha kwanza katika shule ya sekondari Marangu inayomilikiwa na kanisa Katoliki jimbo la Moshi, (jina limehifadhiwa) alitekwa na kukufungiwa kwenye hoteli moja ya kitalii mjini hapa na kufanyiwa vitendo vya ngono kwa muda wa siku nne mfululizo.

Mwanafunzi huyo anadaiwa kutekwa Agosti 6 mwaka huu na kijana mmoja (jina linahifadhiwa) mfanyakazi wa kampuni ya simu za mikononi (Airtel) mjini Dodoma.

Akizungumza jana na Tanzania Daima Jumatano, kaka wa mwanafunzi huyo, Joseph Temba, alidai mdogo wake alitekwa na mtu huyo na tayari mtuhumiwa ameshakamatwa.

Alisema walifanikiwa kumkamata mtuhumiwa huyo Agosti 10, mwaka huu, katika baa moja akiwa na mdogo wake baada ya raia wema kutoa taarifa za kuonekana kwake.

Kwa mujibu wa kaka wa mwanfunzi huyo siku ya tukio alipokea simu kutoka kwa mwangalizi wa wanafunzi (matroni) akimjulisha kutokuwapo bwenini kwa mdogo wake na ndipo walipoanza kufuatilia na kutoa taarifa 
kituo kikuu cha polisi mjini Moshi na kupewa namba Mos/RB/9196/2013.Alisema siku iliyofuata ya Agosti saba jioni walipokea simu kutoka kwa watu wa karibu wakiwataarifu kuwapo katika hoteli hiyo mdogo wake lakini baada ya kufika walinyimwa kuona kitabu cha wageni ili kuangalia orodha ya majina ya wageni waliofikia hapo ili kujiridhisha kama mtuhumiwa huyo alikuwapo mahali hapo.

Hata hivyo alisema jioni ya Agosti 10 walipokea taarifa za kuonekana kwenye baa hiyo mtuhumiwa akiwa na mdogo wake na kuwajulisha polisi na hatimaye kufanikiwa kumtia mbaroni ambapo hadi sasa bado anahojiwa na jeshi la polisi.

Chanzo cha kutekwa kwa mwanafunzi huyo ni mawasiliano ya simu baina ya mtekaji na mwanafunzi huyo ambapo inadaiwa mtuhumiwa huyo alimrubuni mwafunzi huyo kuacha masomo na kwamba angemtafutia nafasi kwenye shule kubwa za kimataifa.

Inadaiwa kwamba mwanfunzi huyo alikubaliana na propaganda hiyo na kutoka shuleni jioni ya Agosti 6 na kumfuata mtuhumiwa kwenye gari lake na kwenda naye hadi Moshi mjini umbali wa kilomteta 50 kutoka shule ya sekondari Marangu.

Kamanda wa polisi mkoa wa Kilimanjaro, Robert Boaz, alisema hana taarifa za kutekwa kwa mwanafunzi huyo kwa kile alichodai alikuwa ametingwa na majukumu ya kikazi mjini Arusha na kuahidi kulifuatilia baadaye.

CHEKA KUZIPIGA NA MMAREKANI AGOSTI 30



KAMPUNI ya 'Hall of Sam B and Promotion Companies' wameandaa pambano la ngumi la dunia uzito wa kati (WBF) kati ya bingwa wa bara la Afrika, Francis Cheka na Philly William wa nchini Marekani litakalofanyika Agosti 30, katika ukumbi wa Diamond Jubilee, Dar es Salaam

Akizungumza Dar es Salaam jana Mratibu wa pambano hilo, Jay Msangi, alisema kuwa pambano hilo litakuwa ni la raundi 12 na uzito wa kilo 76 pamoja na kusindikizwa na mapambano mengine manne.Msangi alisema mbali na pambano hilo pia kutakuwa na mapambano ya utangulizi kati ya Mada Maugo pamoja na Thomas Mashali pambano la raundi 12.
Msangi alisema aliamua kuwakutanisha Maugo na Mashali katika pambano la utangulizi ili kuweza kuvunja majigambo kati ya mabondia hao wawili."Unajua Maugo na Mashali kila mmoja anajigamba kuwa yeye ni bondia bora baada ya Cheka, yaani baada ya Cheka kushika nafasi ya kwanza ya ubingwa wa Afrika wa pili ni wao hivyo swali la jibu hilo nani ni nani litapatikana siku hiyo," alisema Msangi
Pia kutakuwa na pambano la uzito wa juu kati ya Alphonce Mchumia na Deandre McCole wa Marekani, Ibrahimu Classic wa Tanzania atakipiga na Simba wa Tundani wote wa Tanzania na kutakuwa na pambano kati ya Cosmas Cheka na Allan Kamote.
Msangi alisema mpambano huo utukuwa wa kihistoria nchini, hivyo amewataka mashabiki wa mchezo wa ngumi nchini kujitokeza kwa wingi ili kujionea ushindani utakaojitokeza.Viingilio katika pambano hilo litakuwa viti maalum ni sh.150,000, VIP gold 50,000 na 20,000 kwa viti vya kawaida.Tiketi zitaanza kuuzwa kuanzia keshokutwa huku mgeni rasmi katika pambano hilo atakuwa Frankois Botha bingwa mara mbili wa Dunia

Picha zakwanza za Video Ya kukunja Goti Ya MwanaFa & AY ikifanyika Nchini South Afrika,..Bonya hapa kujua zaidi

BRky9_MCAAAQZ6e

PICHA ZA NUSU UCHI ZA DIVA ZAZUA GUMZO,WENGI WADAI ANATAFUTA SOKO "GOLD GIGGER"..!! BONYA HAPA KUJUA ZAIDI

Loveness Diva  sasa  kaamua  kuyapromote  mapaja  yake baada ya  kuchoka  kumpaisha  mpenzi  wake.


Kupitia  account  yake  ya  instagram, jana  Diva  alitupia  picha  ya  paja  lake  na  kuwaacha   mashabiki  wake  wafunguke  kama  paja  lake  ni  zuri  au  baya....

Diddy amuwashia Moto kendrick Lamar kwa vitisho vikali,...Bonya hapa kujua zaidi

Mashambulizi dhidi ya Kendrick Lamar yazidi kuongezeka, hasa pale Diddy alipomuwashia moto kupitia Instagram, nakuthubutu kumuingiza Jay Z kwenye mashambulizi hayo.
Lamar amejikuta katika mashambulizi kutoka kwa Rappers mbali mbali ndani ya masaa 34 baada ya kuvuja kwa ngoma ya Big Sean "Control" ambapo ndani yake kuna mistari yake iliyokuwa ikiwaponda ma-rapper hao na kudai kuwa yeye ni King wa New York.
Diddy ameamua kumshambulia kwa kutumia picha yake akiwa na Jay Z (Mabosi wengine wa NY) wakicheka huku akiambatanisha na maneno yanayomkejeli Kendrick Lamar
"Nakisha Kendrick akasema "mimi ni King wa NewYork"
Diddy sio wa kwanza kumrudishia mashambuliz Lamar, NBA Legend mwenye miaka 67 Phil Jackson aliachia maneno kupitia ukurasa wake wa twitter baada ya Lamar kumtaja kwenye mashairi hayo

Hivi ndivyo alivyopokelewa Feza Kessy baada ya kutua uwanja wa Ndege wa Julias Nyerere, Soma Hapa kujua zaidi


Mwakilishi wa Tanzania katika jumba la Big Brother 'The Chase' aliyetolewa Jumapili Agosti 11 Feza Kessy amewasili leo jioni Tanzania katika uwanja wa kimataifa wa Mwl J.K Nyerere jijini Dar es Salaam.

Katika mapokezi watu mbalimbali walijitokeza kumpokea Feza Kessy akiwemo Vanessa Mdee,Mama mzazi wa Feza kessy,ndugu jamaa na marafiki pamoja na Meneja wa Uhusiano wa Multichoice Tanzania 'Barbara'.


 Rafiki wa karibu sana na Feza anayejulikana kwa jina la Vanessa Mdee nae alikuwepo kumpokea rafiki yake.



Tuesday, August 13, 2013

Hivi ndivyo vitu vinavyochangia kuondoa Radha ya Mapenzi;.. bonya hapa kujua zaidi

VITU HIVI HUONDOA RADHA YA MAPENZI
Tendo la ndoa ni tendo takatifu kwa watu waliooana na linamisingi yake ambayo ikidumishwa hakila kila mmoja atalifurahia. Kuwana baadhi ya wanawake huwa wanajisikia maumivu makali baada ya kufanya tendo la ndoa huwa kama amechanjwa na wembe.
Mara nyingi hali hii husababishwa na mwanaume mwenye kucha ndefu pindi anapokuwa katika harakati za kumwandaa. Kucha hizi kama utaziingiza sehemu za siri kwa mwanamke lazima zitamchubua na kufanya ahisi maumivu wakati wa kufanya tendo.
Mikono mikavu ambayo imeota sugu huwa kama msasa ambao humuumiza mwenzako na kusababisha michubuko kwa ndani.Vile vile unapokuwa na magonjwa ya zinaa ambayo husababisha vidonda kwa ndani na kukufanya uhisi maumivu wakati wa tendo na kushindwa kulifurahia zaidi ya maumivu muda wote.
Kingine ni kikwapa watu wengi hujisahau na kujikuta hawaheshimu tendo hili hata bila kuoga yeye anaingia kazini na kujikuta akiharibu hali ya hewa kutokana na harufu kali itokanayo na jasho la kutwa nzima.
Mara nyingi unatakiwa kuwa msafi wa mwili muda wote kwa kunyoa nywele sehemu za siri, kukata kucha huku ukihakikisha mikono yako ni misafi na laini, kuangalia afya yako kila wakati na kutibu magonjwa ya zinaa yanapokutokea, pia kuoga kabla ya tendo ili kuondoa jasho la kutwa nzima. Ni vizuri kama hujaoa ili kujiepusha na maradhi ya kuambukiza utumie kondomu kwa ajili ya kujikinga.
Tujenge utamaduni wa kuheshimu tendo la ndoa ambalo maandalizi yake yanahitaji mtu kuwa msafi tena mwenye afya bora. Nina imani mtu akizingatia yote haya ataweza kufurahia tendo lake la ndoa.

Monday, August 12, 2013

LUIS SUAREZ, AGOMA KUOMBA RADHI LIVERPOOL NA YUKO TAYARI KUFANYA MAZOEZI PEKE YAKE MILELE


clip_image001Kivyake: Suarez amelazimishwa kufanya mazoezi peke yake na ataendelea kufanya hivyo hadi aombe radhiclip_image001[6]Hasira: Kocha wa Liverpool, Brendan Rodgers amesema Luis Suarez hataruhusiwa kujiunga na kikosi chake hadi aombe radhi
UHUSIANO wa Luis Suarez na Liverpool utaingia katika hatua nyingine wiki hii, baada ya mshambuliaji huyo kukataa kuiomba radhi klabu kwa kauli zake kwamba alikubaliana na kocha ataondoka, kulazimisha kutimkia Arsenal.
Vyanzo vya karibu na mwanasoka huyo wa Uruguay vinaamini uhusiano wake na kocha Brendan Rodgers umeharibika kutokana na kutaka kuondoka Merseysiders kipindi hiki.
Suarez anafanya mazoezi peke yake kwenye viwanja vya mazoezi vya Liverpool, Melwood, na Rodgers amesema hatamruhusu kujiunga na timu yake hadi aombe radhi kwa kauli yake ya wiki iliyopita, akiweka wazi anataka kuhamia Emirates.
Lakini kupitia Sportsmail inafahamu kwamba Suarez hataomba radhi, akiamini amesalitiwa na kocha Rodgers juu ya makubaliano waliyofikia.
Anaamini wamekiuka makubaliano ya kiungwan waliyofikia kwamba, Liverpool, isipofuzu Ligi ya Mabingwa ataruhusiwa kuondoka.
clip_image001[9]Anasotea kifaa: Kocha wa Arsenal, Arsene Wenger tayari ofa zake mbili za kumnunua Luis Suarez zimepigwa chini Liverpool
Arsenal tayari imetoa ofa ya Pauni 40,000,001 kwa ajili ya kumnunua mchezaji huyo, lakini imepigwa chini

Luis Gustavo,. Anukia Arsenal baada ya kusema anahitaji kucheza zaidi katika kikosi cha kwanza,..Soma hapa


clip_image001Arsenal inakaribia kukamilisha usajili wa kiungo wa kimataifa wa Brazil Luis Gustavo toka klabu ya Bayern Munich .
Arsenal na Munich zimefikia makubaliano juu ya bei ya kiungo huyo ambayo itakuwa euro milioni 20 kabla ya kufanya mazungumzo na mchezaji mwenyewe .
Gustavo aliambiwa wazi na kocha wa Bayern Pep Guardiola kuwa hataweza kupata nafasi ya kudumu kwenye kikosi cha kwanza hali inayomfanya atafute timu ya kwenda ambayo itamhakikishia nafasi kwenye kikosi chake .

clip_image001[5]Endapo usajili huu utakamilika utakuwa na ahueni kubwa kwa mashabiki wa Arsenal ambao wamekuwa kwenye huzuni baada ya kumkosa mshambuliaji Gonzalo Higuain ambaye kwa muda mrefu alidhaniwa kuwa mbioni kujiunga na Arsenal kabla ya kujiunga na Napoli .
Pamoja na Higuain Arsenal imeshuhudia ofa zake mbili za kumsajili mshambuliaji Luis Suarez zikikataliwa na Liverpool ambayo imeshikilia uamuzi wa kutomuuza mshambuliaji huyo .
Hadi sasa Arsenal imesajili mchezaji mmoja pekee ambaye ni mchezaji wa timu ya vijana ya Ufaransa Yaya Sanogo

Walter Chilambo."Ney wa Mitego hayajui maisha yangu na hakufikilia kabra ya kunitaja katika wimbo wake...Soma hapa

 Baada ya maneno na tuhuma nzito za Ney wa Mitego dhidi ya Mshindi wa Epiq Bongo Star Search mwaka 2012, Walter Chilambo kuwa 'huenda' amedhulumiwa zawadi yake ya ushindi, Shilingi Milioni 50 na waratibu wa shindano hilo kwa sababu mpaka sasa yupo katika maisha duni, Msanii huyu amevunja ukimya na kusema kuwa yeye yupo vizuri tu.

Walter amesema kuwa maneno haya hayana ukweli wowote na yeye anaishi vizuri tu na kwa Ney, Hadhani kama alikaa chini na kufikiria kabla ya kuongea kuhusiana na issue hii katika wimbo wake, wala hakufanya uchunguzi wowote ambao uliomhusisha yeye.
Walter amesema kuwa yeye na Ney hawana ukaribu wowote, na walishawahi kukutana hivi karibuni na alipomuuliza ni kwanini amemuimba vile katika wimbo wake, Ney alimwambia kuwa 'asipanik' then akapotezea na mambo issue nyingine na kisha kutimua zake.
Walter amemaliza kwa kusema kuwa, Maneno haya hayamuumizi vile hayana ukweli wowote, na vilevile hayawezi kumuondolea mashabiki wake.

Huyu ndiye Marehem aliyenyanyuka katika Jeneza na Kumpora Muombolezaji Chupa ya Maji, Kiu "Chamfufua"


Wapita Njia walipata hali ya  kutishwa wakati mtu huyo, ambaye alisemekana kuwa maiti, ghafla aliamka na kumpora mmoja wa waombolezaji chupa ya maji na kuanza kunywa.

Raia huyo wa China alidanganya kifo chake mwenyewe ili kuishitaki serikali baada ya mabishano na wafanyakazi wa serikali ambao inasemekana walimpiga, basi akafanya uongo huo ili apate fidia ya Kifo hicho.
Lakini mpango wake uliingia dosari kutokana na Hali ya Joto Kali katika Mkoa wa Hubei, Huko China ya kati. 
Tukio hilo lilitokea majira ya saa Kumi Alasiri wakati zaidi ya watu 10 wakiwa wamembeba maiti huyo huku akiwa kufunikwa na karatasi nyeupe karibu na kituo cha Jianghan Road Subway katika mji mkuu wa mkoa wa Wuhan. 
Zaidi ya watu 300 waliokusanyika katika eneo la tukio, na maafisa wa polisi 80 walipelekwa eneo la tukio ili kudumisha amani. 
Baada ya masaa mawili ya maandamano, "Maiti" Mtu huyo ghafla alisimama, akaipora chupa ya maji ya kunywa na  kusema: "Ni Joto sana, siwezi kuvumilia ". 
Maiti huyo aitwaye Han, pamoja na wenzake wawili wengine, wamekamatwa kwa kitendo chao hicho

Huyu ndiye msichana aliye fariki Dunia baada ya kupewa sumu na mtu aliyefahamiana naye Facebook,.. bonya hapa


Msichana mmoja mwenye umri wa miaka 23 ambaye alikuwa anasoma sheria katika chuo kikuu amekumbwa na mauti baada ya kwenda kulala na mtu mmoja tajiri asiyejulikana katika hoteli. Msichana huyo amekutana na tajiri huyo katika internet [facebook]. Kabla ya kwenda huko, wasichana wenzie anaoishi nao chumba kimoja walimktaza kutokwenda, lakini binti huyo alisisitiza. Asubuhi iliyofiata, msichana huyo alikutwa amekufa [pichani]. Chanzo kinadai kuwa, msichana huyo amelishwa sumu. Haya ni matokeo ya ubishi na endapo angaliwasikiliza wenzie jambo hili lisingalimkuta.

Sunday, August 11, 2013

Danguro la uchi lafumuliwa Buguruni, Dar; gharama ya chumba ni 1,200/= kumlipa malaya 5,000 ,,Bonya hapa kujua zaidi

JUMBA linalodaiwa kutumika kuendesha shughuli za ukahaba limebainika kuwapo katika eneo la Buguruni, jijini Dar es Salaam.

Uchunguzi uliofanywa na Tanzania Daima, umebaini kuwapo kwa jumba ambalo linatu
mika kama nyumba ya kulala wageni, ambako idadi kubwa ya makahaba hujazana na kuendesha biashara ya kuuza miili yao bila wasiwasi. 


Wasichana wanaofanya biashara hizo hutoza kiasi cha sh 5,000 kama huduma ya ngono na chumba kwa matumizi ya muda mfupi.

Biashara hiyo ambayo imeleta usumbufu mkubwa kwa wakazi wengi wanaopakana na nyumba hiyo, imekuwa

ikifanikiwa kutokana na kuwapo kwa baadhi ya askari polisi wanaodaiwa kuwalinda wasichana hao pamoja na mmiliki wa nyumba hiyo.

Nyumba hiyo inavyo vyumba vingi vinavyotozwa kiasi sha sh 1,200 kwa chumba pamoja na kondomu. Kadhalika wasichana wenye umri wa miaka 15, ni miongoni mwa wanaofanya biashara hiyo.

Mjumbe wa serikali ya mtaa wa eneo hilo, Amiri Banza, alikiri kuwapo kwa biashara hiyo, ingawa alisema wamejaribu sana kuzuia hali hiyo bila mafanikio: 

“Tumechoka na hii kadhia, tumeripoti kwa viongozi wa Kata hadi polisi lakini hakuna hatua yoyote iliyochukuliwa. Kama wakija polisi wanawakamata, halafu wanawaachia,” alisema.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa kipolisi wa Ilala, Marietha Minangi alipoulizwa juu ya kuwapo kwa jumba hilo alisema hajui chochote.:“Mimi sijapata taarifa hizo na ndiyo kwanza ninakusikia wewe,” alisema.

Alipoulizwa kuhusu polisi kufika kwenye jumba hilo na kuchukua rushwa na kuondoka alisema: “Sina ushahidi, kama wapo polisi wanafanya hivyo ni kosa,” alisema Minangi na kuongeza kuwa polisi wanafanya doria maeneo hayo na mara kadhaa wamewakamata watu wanaojihusisha na vitendo hivyo na kuwafikisha mahakamani.

Yanga funika funua waibamiza SC Villa 4-1 waijibu Simba wakaa nkao wa kula kuisubili Azam,.Soma hapa


YANGA SC imetuma salamu Johannesrbug, Afrika Kusini ambako Azam FC wameweka kambi kujiandaa na msimu mpya- kufuatia ushindi wa mabao 4-1 leo katika mchezo wa kirafiki dhidi SC Villa ya Uganda, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Yanga na Azam zitamenyana Jumamosi ijayo Uwanja wa Taifa, katika mechi ya kuwania Ngao ya Jamii, kuashiria ujio wa msimu mpya wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara.

Azam imeweka kambi Afrika Kusini kujiandaa na mechi hiyo ya kufungua msimu na Yanga wanaendelea na maandalizi yao Dar es Salaam, wakitarajiwa kuingia kambini baada ya mechi ya leo kisiwani Pemba, au Bagamoyo, Pwani.
Katika mchezo wa leo, hadi mapumziko, tayari Yanga SC walikuwa mbele kwa 3-1, mabao yake yakifungwa na Mrisho Ngassa dakika ya saba, Nadir Haroub ‘Cannavaro’ dakika ya 27 na Didier Kavumbangu dakika ya 30, wakati la nne lilifungwa kipindi cha pili na Haruna Niyonzima dakika ya 62.
Bao la kufutia machozi la Villa ambayo jana ilifungwa 4-1 pia na Simba Uwanja huo huo wa Taifa, lilifungwa na Moses Ndaula dakika ya 18.   

Katika mechi zake za awali za kujiandaa na msimu, Yanga SC ilitoa sare ya 2-2 na URA ya Uganda kabla ya kuzifunga 3-1 Mtibwa Sugar na 3Pillars ya Nigeria 1-0. 

Azam nayo imekwishacheza mechi tatu za kujipima nguvu Afrika Kusini, imeshinda moja tu dhidi ya Mamelodi Sundwons 1-0, imefungwa mbili, 3-0 na Kaizer Chiefs na 2-1 na Orlando Pirates na kesho itacheza mechi ya mwisho na Moroka Swallows kabla ya kurejea nyumbani keshokutwa.

Kikosi cha Yanga SC leo kilikuwa; Ally Mustafa ‘Barthez’, Juma Abdul, David Luhende/Oscar Joshua, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Kevin Yondan/Rajab Zahir, Athumani Iddi ‘Chuji’/Bakari Masoud, Mrisho Ngassa, Salum Telela, Didier Kavumbangu, Jerry Tegete/Hussein Javu na Haruna Niyonzima/Said Bahanuzi.

Dimpozi afanya kitu mbaya Burundi amjibu Dimond kwa vitendo, Bonya hapa kujua zaidi

Ommy Dimpoz licha ya kukwama kwa muda kidogo kwenye Airport ya Jomo Kenyatta, hatimaye aliweza kufika nchini Burundi na kufanya show. Baada ya kufika Burundi,  njiani kuelekea kwenye show Ommy Dimpoz alifuatwa na kundi kubwa la watu wakifuatilia gari lake huku yeye akiwapungia mkono. Cheki hii picha kutoka kwake mwenyewe Ommy DimpozommyAhsante kwa kuwa rafiki mkubwa wa Jonstwice.blogspot.com

Kunyonyana ndimi kunaongeza Chachu ya mapenzi ila Unajua madhara yake ? Bonya hapa kujua zaidi....



Kubusiana kwa kunyonyana ndimi kunaweza kuchangia maambukizi ya virusi vya UKIMWI?
Uwezekano wa kuambukizwa virusi vya UKIMWI kwa kunyonyana ndimi ni mdogo sana.Kwa kubadilishana mate wakati wa kubusiana tu, haiwezekani maambukizo ya virusi vya UKIMWI kutokea. Lakini kama mmoja kati ya wapenzi ana vidonda au michubuko mdomoni, uwezekano wa kuambukizana huongezeka.

AJALI YA BASI LA MERIDIANI ENEO LA MBWEWE BASI LIMEKATIKA NA SITI ZIPO NJE.


Bai la Merdiani lililokuwa limetoka Rombo kwenda Dar. Limeanguka hapa karibu na mbwewe . Watu wamekufa. Basi limekatika siti zipo njee. Dereva bado hajatolewa. taarifa zinasema dereva wake kafia hapo hapo na abiria wengine pia wamefariki
                           Ahsante kwa kuitembelea Jontwice.blogspot.com
 

Hivi ndivyo Man United ilivyonyakua Community Shield,, Bonya hapa kujua zaidi

Meneja mpya wa United Moyes alitumia muda wake mrefu katika mazungumzo juu ya hatma ya mashambuliaji Wayne Rooney,lakini uwanjani amekuwa
mshambuliaji Van Persie aliyefunga magoli mengi msimu uliopita ambaye tena ameiwezesha timu hiyo kuibuka mshindi.
Mchezo ulipoanza, imemchukua dakika 6 tu Van Persie kunusa nyavu kwa kuunganisha kwa kichwa mpira uliopigwa na mlinzi wa kushoto, Patrice Evra.
Wigan ambayo sasa inacheza katika daraja la pili,imejaribu kutishia ngome ya United bila mafanikio kwani walinzi wake walionekana kudhibiti vilivyo sehemu zao uwanjani.
United walijihakikishia kuondoka na ushindi kunako dakika ya 59 ambapo pia amekuwa mshambuliaji Van Persie aliyetikisa wavu kwa mkwaju wake uliopiga kwenye mguu wa mlinzi wa Wigan na kumhadaa mlinda lango.
Ushindi huo wa Manchester United wa magoli 2-0 ametosha kwa meneja mpya David Moyes kusherehekea kombe la community Shield,kombe lake la kwanza.
Baada ya ushindi huo sasa macho yanaelekezwa upande wa ligi kuu ambapo United wataanza kampeni ya kutetea taji lao ugenini dhidi ya Swansea siku ya jumamosi

HIZI NDIZO PICHA ZA SHEKH PONDA AKIWA HOSPITALINI AKISUBIRI MATIBABU BAADA YA KUPIGWA RISASI




Sheikh Ponda leo akiwa HOSPITALINI akisubiri matibabu baada ya kupigwa Risasi huko Morogoro

HUYU NDIYE MTANZANIA MREFU KULIKO WOTE TANZANIA ANAMZIDI HATA HASHIMU THABITI, bonya ha kujua zaidi

Huyu ni Baraka kijana mrefu  kitanzania


Inasemekana ni kijana mrefu kuliko wote Tanzania. Kijana huyu (katikati pichani) ambaye anadhaniwa ni mrefu kuliko vijana wote Tanzania anaishi maeneo ya Gongolamboto, Banana jijini Dar es salaam. Kijana huyu huwa haonekani sana mitaani, lakini aliingia mjini siku hiyo na kuleta kizaa zaa kikubwa pale alipoibuka mitaa ya Aggrey, Kariakoo. Alikuwa kivutio kwa kila aliyemuona, alifunga mtaa watu wakimshangaa na kumgombania kupiga nae picha. Kila aliyetaka kupiga nae picha alitoa Shilingi elfu moja Tsh. 1000.

Picha hiyo amepigwa ndani ya Kinyozi (Salon) aliyoingia kupunguza nywele zake na umati wa watu walikuwa nje ya kinyozi huyo kumsubiri atoke. Mpaka sasa hajajulikana jina lake kamili na anafanya nini. Inasemekana kuna watu wanamfuatilia kumsaidia umaarufu.

Hapa Hasheem Thabit alipokutana na Baraka
 
JULIUS CHARLES
UKIMUANGALIA kwa mara ya kwanza mchezaji wa Tanzania anayecheza timu ya kikapu ya Oklahoma City Sounders inayoshiriki Ligi ya Kikapu Marekani (NBA), Hasheem Thabit unaweza kujiridhisha kwamba ni mrefu kuliko Watanzania wote uliowahi kuwaona. Ana futi 7.3.
Lakini mjini Bagamoyo katika Mkoa wa Pwani kwenye shule ya Lord Barden yupo mchezaji anayemzidi Hasheem kwa urefu akiwa na futi 7.5. Si mwingine namzungumzia Julius Charles (18) ni maarufu zaidi maeneo ya Bagamoyo, na umaarufu huo umetokana na kimo chake huku wengi wakimuita mpinzani wa Hasheem Thabit  kutokana na urefu alionao ambao umepitiliza na ukikutana naye lazima utishike au ubaki ukimshangaa

HII NDIYO BARUA KWA KIKWETE ILIYO ANDIKWA NA BATULI KUHUSU BONGO MOVIE,..bonya hapa kujua zaidi

 
Yobnesh Yusuph(Batuli) ambaye ni actress maarufu Swahiliwood amemuomba Rais Jakaya Kikwete alivunje Baraza la Sanaa la Taifa(BASATA) na kuliunda upya. Leo kupitia akaunti yake ya twitter muigizaji huyo aliyejaaliwa mvuto na kupendwa na mashabiki wengi wa filamu ali-tweet moja kwa moja akimtaja JK kwa kuandika "ujumbe wa sikukuu ya Eid kwako Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzana, vunja baraza la BASATA uliunde upya".
Ingawa Batuli hakutaja moja kwa moja kwanini baraza hilo linalosimamia sanaa ikiwemo tasnia ya filamu nchini livunjwe lakini kwa muda mrefu wasanii wakiwemo wa filamu na muziki wamekuwa wakililalamikia baraza hilo kuwa linafanya mambo kienyeji na baadhi ya wasanii kudai kukumbana na urasimu wanapotaka kufanya kazi zao za sanaa.
Wengine wanadai hata hatua iliyopigwa sasa katika sanaa nchini ni juhudi za wasanii wenyewe pasipo sapoti ya kutosha kutoka BASATA. Baadhi ya wasanii wa filamu wamekuwa pia wakitaka TAFF ndiyo ipewe mamlaka kamili ya kusimamia shughuli zote za tasnia ya filamu nchini kutokana na BASATAkuwepo muda mrefu lakini Sanaa ya Tanzania bado haijapewa hadhi ya sekta rasmi na kuwa na sera ya kueleweka katika kumkomboa msanii na kuzidi kupiga hatua.
Hivi karibuni pia mwanamuziki Diamond Platinumz alikaririwa akisema BASATA ndiyo wa kulaumiwa kwa kutokuwa na tuzo nyingine za muziki mpaka sasa kwa kuwa chombo hicho kimekuwa kikiweka kauzibe kwa watu wanaotaka kuazisha tuzo mbalimbali za sanaa ikiwemo hata katika tasnia ya filamu

Soma hapa alichokisema Zito kabwe baada ya shekh Ponda kushambuliwa huko Morogoro....Bonya hapa kujua zaidi


Saturday, August 10, 2013

UKATILI,.BABA AMLAWITI MTOTO WAKE WA KIUME NA KUMBAKA SHEMEJI YAKE JIJINI DAR


clip_image001Binti aliyebakwa akiwa na mtoto aliyelawitiwa.
MWANAUME aliyefahamika kwa jina moja la Mohammed, mkazi wa Kigamboni jijini Dar amedaiwa kuwafanyia unyama watoto wawili, akimlawiti mwanaye wa kufikia na kumbaka mdogo wa mkewe...
Akizungumza na mwandishi wetu  juzi nyumbani kwake, mke wa mtuhumiwa huyo, Zubeda alisema watoto waliofanyiwa hivyo ni mwanaye wa kiume (6) na mdogo wake wa kike (16) (majina tunayo).
Mwanamke huyo alisema: Nilikutana na Mohammed nikiwa na mtoto huyo wa kiume, ndani  ya uhusiano wetu tukajaliwa kupata mtoto wa kiume hivi karibuni, hapo ndipo matatizo yalipoanza.
“Alihama chumba ili mimi nilale na kichanga, akaenda kulala na mtoto huyo. Niliamini angemchukulia kama mwanaye kwa kuwa tulishaoana.

Baadhi ya majirani wakiwa na huzuni
“Mwaka jana alikuja mdogo wangu, tukabadili kulala, tuliwaacha watoto hao walale chumba kimoja mume wangu akarudi chumbani. Alizua tabia ya kutoka usiku eti kuvuta sigara kumbe alikuwa anakwenda kumwingilia mdogo wangu,” alizidi kudai mwanamke huyo.
  Alidai kuwa ikafika wakati akagundua mwanaye huyo anajisaidia kwenye nguo na kinyesi kinakuwa na damu, akawa anampiga na kumwamuru afue nguo mwenyewe.
  “Juzi shoga yangu mmoja alikuja akaniambia amemsikia  mume wangu akitamba baa kwamba amemtoa ‘usichana’ mdogo wangu.
“Nilimuuliza mtoto wangu ambapo aliniambia ni kweli baba yake amekuwa akienda chumbani kwao na kumfanyia mchezo mbaya.
“Ukweli taarifa hizo zilinishtua sana, sikutarajia mdogo wangu kama angeweza kulala na mume wangu, nilimpiga sana.
“Wakati namwadhibu mtoto wangu naye akaona kumbe kitendo kile ni kibaya akasema hata yeye baba yake amekuwa akimfanyia mchezo mchafu kila siku usiku,” alisema mama huyo huku akilia.
Wakati watoto hao wakikiri kufanyiwa hivyo, Mohammed alikuwa akiwasikia na kujitetea kwamba walikuwa wakimsingizia, ghafla alipokea simu na kusema anakwenda kwenye biashara akirudi watazungumzia suala hilo lakini hakurudi tena.
Baada ya kuona hivyo, mke huyo alikwenda kutoa taarifa katika Kituo cha Polisi cha Kigamboni na kufungua kesi mbili zenye namba KGD/RB/5218/2013 KUBAKA na KGD/RB/5244/2013 KULAWITI, mpaka sasa mtuhumiwa huyo anasakwa na polisi.
Mwanamke huyo alisema alipewa PF3 na kuwapeleka waathirika hao Hospitali ya Vijibweni na vipimo vilionesha waliharibiwa sehemu zao za siri.
Mama huyo alisema daktari amemwambia mtoto wake wa kiume angeweza kupoteza uhai kama angeendelea kufanyiwa mchezo huo.

Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Mji Mwema, Mwinyi Baishe alithibitisha kusikia madai hayo.

Hii ndiyo Range Roversport iliyo teketea kwa Moto kutokana na wivu wa mapenzi, Bonya hapa kujua zaidi...


Wivu noma sana , Dada mmoja huko Mbezi amelitia Kiberiti Gari la mpenzi wake aina ya Range Rover Jipyaaa Baada ya kukuta Condom iliyotumika kwenye gari hilo , Mashahidi wanasema wakati analiwasha moto alikuwa akisema kuwa hilo gari ndio linakutia kiburi mpaka kutembea na wanawake zako ndani ya gari , tuone sasa ukitaka katembee nao vichakani....
Whats your take ?

Picha za DIAMOND akipiga show yake Nairobi na Kuaacha gumzo kubwa nchini Kenya, Bonya hapa kujua zaidi


Ni jambo jema kumshukuru Mungu kwa kumaliza mfungo
huu wa Ramadhani pia kutuweka salama hadi leo...
Sikukuu yangu nimeilia nchi Kenya lakini nilikuwa na
kibarua kukonga nyoyo za maelfu ya mashabiki zangu
jijini Nairobi.Kwangu hii ilikuwa mara ya pili kufanya show
 kenya,lakini ni mara ya kwanza kabisa
kufanya show jijini Nairobi,kutokana na kiu ya mashabiki
 zangu nchini humo nikaona zawadi ya Eid hii
iwadondoke wao.....It was crayzz yanii niliposhuudia umati wa
 watu wakiimba nyimbo sambamba na mimi,na kufurika hadi getini
kiukweli nilifurahi sana kwa hali iliyokuwa usiku wa jana.....
Nikiwa na team yangu nzima ya wasafi,stejini na
silaha zangu 4 hatari kwenye Mashine alikuwepo
Dj Rommy Jones kama kawaida stage manager
Qboy msafii alikuwepo kuhakikisha usalama upo saawia kabisa.....!!

UNAWEZA CHEKI PICHA KADHAA ZA TUKIO ZIMA
 LA SHOW NCHINI KENYA
KWENYE SIKUKUU YA EID...
..
Backstage nikisubiria go ahead nikafanye maujanja yangu kwa steji...
Ajajajaja....hapo sasa,ndo vile twafanyaga kwa jukwaaaa.....

Qboy Msafii & Dj Rommy Jones...

Ebhana eeeh watu bado wanataka niendeleee.....mpera mpera
 tu,afe kipa afe beki lakini ushindi lazima


Siwasiki watu wangu wa Nairobi.....nimekuja kuwabamba ile mbaya....
Tumeelewana watu wangu wa kweli........Mi naona kama muda umeisha vile....
Si ndo mashetani ya kigoma yakapanda ni kuanza kuwapelekea
kama Bongo tu...
Duuh Ebhana eeeeehhh.....NIMEMALIZA......