Meneja mpya wa
United Moyes alitumia muda wake mrefu katika mazungumzo juu ya hatma ya
mashambuliaji Wayne Rooney,lakini uwanjani amekuwa
mshambuliaji Van Persie aliyefunga magoli mengi msimu uliopita ambaye tena ameiwezesha timu hiyo kuibuka mshindi.
mshambuliaji Van Persie aliyefunga magoli mengi msimu uliopita ambaye tena ameiwezesha timu hiyo kuibuka mshindi.
Mchezo ulipoanza,
imemchukua dakika 6 tu Van Persie kunusa nyavu kwa kuunganisha kwa
kichwa mpira uliopigwa na mlinzi wa kushoto, Patrice Evra.
Wigan ambayo sasa
inacheza katika daraja la pili,imejaribu kutishia ngome ya United bila
mafanikio kwani walinzi wake walionekana kudhibiti vilivyo sehemu zao
uwanjani.
United
walijihakikishia kuondoka na ushindi kunako dakika ya 59 ambapo pia
amekuwa mshambuliaji Van Persie aliyetikisa wavu kwa mkwaju wake
uliopiga kwenye mguu wa mlinzi wa Wigan na kumhadaa mlinda lango.
Ushindi huo wa
Manchester United wa magoli 2-0 ametosha kwa meneja mpya David Moyes
kusherehekea kombe la community Shield,kombe lake la kwanza.
Baada ya ushindi
huo sasa macho yanaelekezwa upande wa ligi kuu ambapo United wataanza
kampeni ya kutetea taji lao ugenini dhidi ya Swansea siku ya jumamosi
No comments:
Post a Comment