Hivi ndivyo vitu vinavyochangia kuondoa Radha ya Mapenzi;.. bonya hapa kujua zaidi
VITU HIVI HUONDOA RADHA YA MAPENZI
Tendo la ndoa ni tendo takatifu kwa watu waliooana na linamisingi yake
ambayo ikidumishwa hakila kila mmoja atalifurahia. Kuwana baadhi ya
wanawake huwa wanajisikia maumivu makali baada ya kufanya tendo la ndoa
huwa kama amechanjwa na wembe.
Mara nyingi hali hii husababishwa na
mwanaume mwenye kucha ndefu pindi anapokuwa katika harakati za
kumwandaa. Kucha hizi kama utaziingiza sehemu za siri kwa mwanamke
lazima zitamchubua na kufanya ahisi maumivu wakati wa kufanya tendo.
Mikono mikavu ambayo imeota sugu huwa kama msasa ambao humuumiza
mwenzako na kusababisha michubuko kwa ndani.Vile vile unapokuwa na
magonjwa ya zinaa ambayo husababisha vidonda kwa ndani na kukufanya
uhisi maumivu wakati wa tendo na kushindwa kulifurahia zaidi ya maumivu
muda wote.
Kingine ni kikwapa watu wengi hujisahau na kujikuta
hawaheshimu tendo hili hata bila kuoga yeye anaingia kazini na kujikuta
akiharibu hali ya hewa kutokana na harufu kali itokanayo na jasho la
kutwa nzima.
Mara nyingi unatakiwa kuwa msafi wa mwili muda wote kwa
kunyoa nywele sehemu za siri, kukata kucha huku ukihakikisha mikono
yako ni misafi na laini, kuangalia afya yako kila wakati na kutibu
magonjwa ya zinaa yanapokutokea, pia kuoga kabla ya tendo ili kuondoa
jasho la kutwa nzima. Ni vizuri kama hujaoa ili kujiepusha na maradhi ya
kuambukiza utumie kondomu kwa ajili ya kujikinga.
Tujenge
utamaduni wa kuheshimu tendo la ndoa ambalo maandalizi yake yanahitaji
mtu kuwa msafi tena mwenye afya bora. Nina imani mtu akizingatia yote
haya ataweza kufurahia tendo lake la ndoa.
No comments:
Post a Comment