GENERATION OF LOVE UNIT

GENERATION OF LOVE UNIT
GENERATION OF LOVE@2013

Friday, August 2, 2013

Baada ya kushindwa Tsvangirai adai uchaguzi Zimbabwe ni kichekesho. Soma hapa kujua zaidi


                                Thanks For Choosing Jonsttwice
Add caption

Waziri Mkuu Morgan Tsvangirai amesema Uchaguzi wa Rais nchini Zimbabwe ulikuwa ‘kichekesho kikubwa’, akituhumu udanganyifu wa kura uliofanywa na kambi ya mpinzani wake Rais Robert Mugabe.
Katika mkutano na waandishi wa habari, Bw Tsvangirai alisema upigaji kura uliofanyika Jumatano ulikuwa ‘upuuzi na si halali’.Waangalizi wa uchaguzi huo wengi wao wamesema karibu watu milioni moja walizuiwa kupiga kura.
Aidha Zanu PF imenukuliwa kudai kushinda,imekanusha tuhuma hizo ikisema upigaji kura ulikuwa shwari.
Kiongozi wa ujumbe wa Umoja wa Afrika, Rais wa zamani wa Nigeria Olusegun Obasanjo, alisema kwenye tathimini yao ya awali kuwa upigaji kura ulikuwa huru na haki.Makundi mengine ya waangalizi yalisifia hali ya amani katika uchaguzi huo.
Shughuli ya kuhesabu kura ilianza usiku na Tume ya Uchaguzi ya Zimbabwe (ZEC) imedai kutangaza matokeo ya uchaguzi huo ndani ya siku tano.
Tayari polisi wameonya kuwa watachukua hatua dhidi ya yeyote atakayejaribu kuvujisha habari za matokeo. Ni kinyume cha sheria kutangaza matokeo yasiyo rasmi.
Mji wa Harare umeenea Vikosi vya ziada vya askari baadhi vikiwa na vifaa vya kupambana na waandamanaji na yeyote atakaye vunja sheria wakati wa kusubiri kutangazwa kwa matokeo rasmi.

No comments:

Post a Comment