GENERATION OF LOVE UNIT

GENERATION OF LOVE UNIT
GENERATION OF LOVE@2013

Saturday, January 25, 2014

Wenger, amshambulia Jose Morinho juu ya usajili wa Mohamed Salah kuchukua mikoba ya Juan Mata. Bonya hapa kujua zaidi


 Green light: The Reds look set to bid for Mohamed Salah

London, England.
 Kocha wa Chelsea, Jose Mourinho ameendelea kufanya mabadiliko katika kikosi chake baada ya juzi kumsajili winga Mohamed Salah kutoka klabu ya Basel.
Taarifa ya klabu ya Chelsea ilisema, “Klabu ya Chelsea inaweza kuthibitisha kwamba tumekubaliana na klabu ya FC Basel na tutamchukua kiungo mshambuliaji wa timu hiyo, Mohamed Salah.”
Kutokana na makubaliano hayo, klabu ya Chelsea inatarajiwa kumtambulisha Salah siku ya Jumapili wakati Chelsea itakapokuwa ikicheza na Stoke mechi ya Kombe la FA raundi ya nne.
Salah atakuwa mchezaji wa tatu kusajiliwa na Chelsea katika kipindi hiki kwani tayari imewasajili wachezaji Betrand Traore na Nemanja Matic. Wachezaji hao wamesajiliwa na Chelsea baada ya kuwauza nyota Kevin De Bruyne na Juan Mata.
Mourinho amemsajili Salah kwa sababu anaona ni mchezaji mbadala anayeweza kuziba pengo la Mata aliyeuzwa katika klabu ya Manchetser United.
Hata hivyo, usajili huo wa Mata kwenda Manchester United umeonekana kumshangaza sana kocha wa Arsenal, Arsene Wenger kwani alisema Chelsea haitaathirika kwa kumuuza Mata ila timu nyingine ndiyo zitaathirika.
Wenger alisema Chelsea wameishacheza na Manchester United nyumbani na ugenini msimu huu kwa hiyo hawataathirika kwa kumuuza Mata.
“Mimi nadhani kipindi hiki cha usajili wa dirisha dogo kingesimamishwa wakati timu zikiwa zimeishakutana mara moja na kumalizika mzunguko wa kwanza,”alisema Wenger.
Kocha Wenger alikanusha taarifa zilizopo kwamba anataka kumsajili mshambuliaji wa Barcelona Cristian Tello kwani alikwenda Hispania kushuhudia mechi kati ya Barcelona dhidi ya Levante.
Hata hivyo, zipo taarifa kwamba Arsenal bado inaendelea na harakati zake za kutaka kumsajili mshambuliaji wa Schalke, Julian Draxler kwa ajili ya kuziba pengo la mshambuliaji wake Theo Walcott aliyeumia goti.

No comments:

Post a Comment