GENERATION OF LOVE UNIT

GENERATION OF LOVE UNIT
GENERATION OF LOVE@2013

Friday, August 9, 2013

Matumaini akisema kilicho taka kumuua huko Msumbiji nakutangaza kurudi kazini Rasmi. Soma hapa

Afya ya Matumaini yaimarika na ameanza kurejea katika fani yake


BAADA ya kutoka nchini Msumbiji akiwa hoi, msanii wa vichekesho Bongo, Tumaini Mwakibibi ‘Matumaini’ hatimaye amepata nguvu na ameanza kujikongoja katika kazi ya uigizaji.
 
Akiongea hivi karibuni, Matumaini alisema kwa sasa anaendelea vizuri na ameshaanza kucheza filamu mbalimbali anazoshirikishwa na wasanii wenzake na sasa anaendesha maisha yake mwenyewe.
   
“Nawashukuru sana wasanii wenzangu kwani kama siyo wao, ningerudishwa nikiwa maiti, sina cha kuwalipa ila Mungu ndiye atakayewalipa,” alisema Matumaini.
  
Hata hivyo, amelaani vikali baadhi ya wasanii wanaozusha maneno ya uongo kwamba Michael Sangu alikula fedha alizokuwa anachangisha kwa ajili yake jambo ambalo siyo la kweli.

No comments:

Post a Comment