GENERATION OF LOVE UNIT

GENERATION OF LOVE UNIT
GENERATION OF LOVE@2013

Friday, July 26, 2013

Kaburu Mwenyeketi mpya Simba sc, Atangaza nia na Sababu za kutaka nafasi hiyo. Soma hapa,,,,,,,

Kaimu mwenyekiti wa Simba SC, Godfrey Nyange Kaburu amesema atawania nafasi ya Uenyekiti wa klabu hiyo pindi muda wa Mwenyekiti wa sasa utakapoisha.
Akizungumza na Jonsttwice, Kaburu amesema anajiona mwenye sifa za kuchukua nafasi hiyo na kuingoza timu hiyo yenye maskani yake mitaa ya Msimbazi.
Kwa sasa timu hiyo ipo chini ya Mbunge wa Tabora Mjini, Mh Aden Rage, ambae katika mkutano wake uliopita na wanachama wa timu hiyo aliwafafanulia suala la uwanja kwa Simba ni ndoto, ingawa pia Kaburu amegusia katika mazungumzo yake kuwa hata Azam FC uwanja wao ni wa Bakhresa na Sio Azam FC.
Lakini ikumbukwe kuwa Azam FC ni sehemu ya Kampuni ya Bakhresa hiyo hiyo, hivyo bado Azam FC inahitaji kujivunia suala la uwanja kama vile mambo mengine yanayohusiana na timu.
Ikumbukwe wadau wengi waliongelea na wamekuwa wakiuliza kwanini Simba na Yanga hazina viwanja wakati Azam FC ina kiwanja? Ukweli ni kwamba timu zote zinahitaji mikakati mathubuti ya muda mrefu, nje ya uwanja na ndani ya uwanja.
Huenda Kaburu akaisaidia Simba isisubiri miaka 50 kujenga uwanja kama kwa mujibu wa kauli ya Mwenyekiti wa Sasa wa simba alivyotamka.
Muda wa Aden Rage unamalizika mwakani.

No comments:

Post a Comment