GENERATION OF LOVE UNIT

GENERATION OF LOVE UNIT
GENERATION OF LOVE@2013

Wednesday, July 31, 2013

Angalia aliyoyasema Nando baada ya kufika Tanzania, mahojiano mafupi tuliyofanya naye.,,,bonya hapa






Maneno mengi yamezungumzwa baada ya Nando kutolewa katika Jumba la Big Brother huko South afrika baada ya kutofautiana na mshiriki mwenzake Alikem raia wa Ghana nakuacha Simanzi kubwa kwa wafatiliaji wa Big brother, Na baada ya Nando kufika Tanzania Jonsttwice ilifanikiwa kufanya naye mahojiano mafupi na hapa anaeleza zaidi….
        Jons, Nando ni Mtu gain ?
    Nando,..Nimtanzania aliye kulia mtaani na kujijengea kuwa na ndoto ya kuwa mtu mkubwa ulimwenguni mwenye mafanikio.
          Jons,..uliwaza nini hadi kushiriki Bigbrother ?
     Nando,..Nia nilikuwa nayo toka zamani yakushiriki sababu unatakiwa uwe na mipango mingi itakayo fanikisha utoke sehem ulipo na kufanikiwa katika maisha hasa ukiwa kijana ikanipelekea kushiriki Big brother msimu huu,
         Jons,..Siku ya kwanza ulipo fika ndani jumba uliwaza kufanya nini kwanza kabra yayote?
      Nando,..kusoma mazingira ya lile jengo na watu waliopo mle ndani maana kamaunavyojua jons watu walikuwa wametoka nchi 14 tofauti kwa hiyo hatujuani kabisa so cha kwanza ni kuwasoma wapinzani wako kabra.
      Jons,.. Ukiwa ndani ulionyesha uwezo wa kusakata soka vipi kuhusu hicho kipaji?
    Nando,.. Yah mpira nilicheza zamani nikiwa hapa Tanzania mechi za mchangani na nikaumia miguu nikiwa ligi daraja la tatu hapa Dar es salaam ikabidi nisimame kucheza hadi nilipo kwenada Amerika nikacheza kidogo bahati mbaya nikaumia tena ndipo nilipo acha Soka kabisa.
     Jons,..nikipi kilicho kutoa Big Brother ?
   Nando,..Nikiwa mle ndani nilifanya vitu vikuu vitatu ambavyo Big hakuvivumilia ikabidi anitimue, kwanza nilienda na kisu katika Party ya Chanel, O kitu ambacho hakitakiwi ila imetokea kuwa mazoea yangu ya kutembea nacho hata nikiwa nyumbani, Pili nikakutwa tena na mkasi na tatu ni ugonvi na Elikem,
    Jons, Nafassi ya Feza kuchukua milioni 500 unaionaje ?
  Nando,..Ushindani upo ila naamini atafanya vizuri na kuwa mshidi ila hawezi kuwa mshidi bila sisi kumpigia kura ili awe mshindi sababu yeye watanzania ndio wameishika nafasi yake mkononi kwa hiyo tupige kura kwa wingi dada yetu ashinde.
        Jons,.. Sasa hivi umerudi nyumbani je hizo milioni ungerudi nazo uliwaza kufanya nini?
  Nando,..Kuinua Entertainment ya Tanzania hasa mziki maana ni kweli tuna maendeleo kiasi ila wenzetu wametupiga gepu kubwa sana kama Nigeria, na nchinyingine mimi nimekaa mle ndani nimesikia Nyimbo ya Feza tu ikipigwa kwa wasanii wetu wa Tanzania tena siku moja rabda na za Kenya chache ila nyingi ni za wenzetu sasa niliwaza kuja kuinua mziki wetu wa hapa Bongo.
     Jons,.. Unakipi cha mwisho kwa mashabiki wako ?
   Nando,.. Wasahau yaliyo tokea na kuungana wote kumpigia kura Feza, tuamini yeye bila sisi hatashinda cha kufanya ni kuandika Vote Feza kwenda 15456 tutume zaidi na zaidi.

No comments:

Post a Comment