Masanduku ya kupigia kura
Matokeo ya awali ya uchaguzi
mkuu nchini Zimbabwe yanadhihirisha chama cha Rais Robert Mugabe,
ZANU-PF kinaongoza.Chama hicho tayari kimedai ushindi. Msemaji wa chama
hicho Rugare Gumbo alisema chama hicho kilitarajiwa kushinda kiasi ya
asilimia 70 ya kura hizo.
Lakini mpinzani wa Mugabe, Morgan Tsvangirai,
amesema uchaguzi huo ni wa uongo na kusema udanganyifu uliofanyika una
maana uchaguzi huo haukubaliki.Waangalizi kutoka Umoja wa Afrika na jumuia ya maendeleo kusini mwa Afrika wanatarajiwa kutoa tamko rasmi hii leo kuhusu uchaguzi huo.
Mkuu wa waangalizi kutoka Umoja wa Afrika alisema tathmini yake ya awali ni kuwa uchaguzi huo ulikuwa wa huru na wa haki.
No comments:
Post a Comment